Katika tafiti nyingi zilizofanya, iligundulika kuwa watu wengi kutoka nchi zinazoendelea hawafahamu hali za afya zao. Hii ni kutokana na kutofanya vipimo vya mara kwa mara kuangalia hali za afya. Kwa jinsi mwili unavyofanya kazi, na jinsi ulivyo na sehemu nyingi, ni vyema tukawa na desturi ya kupima afya zetu mara kwa mara.